Matamshi ya Shurti katika Nuru
Matamshi ya shurti katika Nuru yanatumika kutekeleza utendaji tofauti kulingana na masharti fulani. Tamshi la kama/sivyo muundo wa msingi kudhibiti ambao unakuwezesha kutekeleza msimbo kwa kulingana na masharti maalum. Ukurasa huu unaangazia misingi ya tamshi la kama/sivyo katika Nuru.
Kama
Tamshi la kama linaanza na neno msingi kama
, likifuatiwa na mabano ya sharti. Kama sharti ni kweli, msimbo ndani ya mabano singasinga utatekelezwa.
kama (2 > 1) {
andika(kweli) // Tokeo: kweli
}
kama (2 > 1) {
andika(kweli) // Tokeo: kweli
}
Katika huu mfano, sharti 2 > 1
ni kweli, hivyo tamshi la andika(kweli)
litatekelezwa na tokeo litakua kweli
.
Au Kama na Sivyo
Unaweza kutumia au kama
kujaribisha masharti mengi na sivyo
kubainisha pande la msimbo litakalotekelezwa pale ambapo masharti yote sio kweli.
fanya a = 10
kama (a > 100) {
andika("a imezidi 100")
} au kama (a < 10) {
andika("a ndogo kuliko 10")
} sivyo {
andika("Thamani ya a ni", a)
}
// Tokeo litakua: 'Thamani ya a ni 10'
fanya a = 10
kama (a > 100) {
andika("a imezidi 100")
} au kama (a < 10) {
andika("a ndogo kuliko 10")
} sivyo {
andika("Thamani ya a ni", a)
}
// Tokeo litakua: 'Thamani ya a ni 10'
Katika huu mfano, sharti la kwanza a > 100
sikweli, na kwenye sharti la pili a < 10
pia sikweli. Hivyo basi, msimbo ndani ya pande la sivyo
unatekelezwa, na tokeo ni "Thamani ya a ni 10".
Kwa kutumia matamshi ya kama/sivyo ikiwa na maneno msingi kama
, au kama
, na sivyo
, utaweza kudhibiti mtiririko wa msimbo wako wa Nuru kwa kuzingatia masharti tofauti.